SOMA ZAIDI.....Raia mmoja wa china, Xiaolian mwenye miaka 22 amefanyiwa matibabu ya kutengeneza pua mpya ambayo itachukua nafasi ya pua yake ambayo ilipata madhara alipopata ajali ya barabarani.
Xiaolian Ameoteshwa pua kwenye paji la uso wake baada ya wataalam kushindwa kuiponya ile iliyoharibika baada ya ajali.
Utengenezaji wa pua hiyo mpya, umefanywa kwa kuchukua sehemu ya mbavu za binadamu kwa kukatwa kwa muundo wa pua.
Madaktari wamesema mwanaume huyo anaendelea vizuri na zoezi la kuipandikiza pua hiyo mpya eneo la pua ya zamani utafanyika hivi karibuni.