facebook likes

Thursday, July 4, 2013

Chelsea wamemsajili huyu nyota wa Uholanzi aisee




Marco Van Ginkel.
Marco Van Ginkel.
Klabu ya Chelsea imefikia makubaliano rasmi ya kumsajili nyota wa timu ya taifa ya Uholanzi kwa vijana wenye umri chini ya miaka 21 Marco Van Ginkel toka klabu ya Vittesse Arnherm . Nyota huyo atathibitishwa kuwa mchezaji wa Chelsea ndani ya siku chache zijazo baada ya ofa toka kwa The Blues ya Euro milioni 10.5 kukubaliwa na klabu ya Vittesse.
Usajili wa Van Ginkel utakamilika baada ya mchezaji huyo kufaulu vipimo vya afya pamoja na makubaliano binafsi baina yake na Chelsea vitu ambavyo kuna uhakika kuwa havitamzuia nyota huyo kuwa mchezaji mpya wa Chelsea .
Kiungo mshambuliaji  huyo aliibuka na kutengeneza vichwa vya habari baada ya kufanya vizuri kwenye msimu wake wa kwanza kwenye klabu yake ambapo alifuga mabao nane kabla ya kufanya vizuri kwenye fainali za Mataifa ya Ulaya kwa vijana wenye umri chini ya miaka 21 na kabla ya hapo alipewa tuzo ya ‘mchezaji mwenye kipaji bora wa mwaka” yaani Talent Of The Year kwenye tuzo za wachezaji bora wa uholanzi kwa msimu ulioisha jambo lililomfanya kocha wa timu ya Taifa ya wakubwa Louis Van Gaal kumuita kwenye kikosi chake ambapo amecheza mechi moja .
Klabu ya Chelsea imepata wepesi wa kumsajili Marco Van Ginkel kutokana na mahusiano mazuri yaliyopo baina ya klabu hiyo na klabu ya Vittese Arnherm ambapo siku za nyuma Chelsea imewahi kuwapa Vittese wachezaji ambao walicheza kwenye klabu hiyo kwa mkopo kama Gael Kakuta na Patrick Van Aanholt.
Van Ginkel anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Chelsea chini ya utawala wa kocha mpya aliyerejea kwa mara ya pili Jose Mourinho baada ya Andre Schurle toka Ujerumani huku wachezaji wengine kama Edinson Cavanni na Wayne Rooney wakihusishwa na usajili ndani ya Chelsea.


No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...