facebook likes

Thursday, July 4, 2013

Ryan Giggs si amepewa cheo kipya Manchester United leo aisee.. ni cheo gani?



ryan-giggs-football-sport-celebrity
Kiungo/winga wa muda mrefu wa klabu ya Manchester United Ryan Giggs ameteuliwa kuwa kocha mchezaji ndani ya klabu hiyo ambapo atakuwa akisaidiana na kocha David Moyes pamoja na makocha wengine wasaidizi .
Mchezaji huyo ambaye amekuwa na United kwa misimu 23 akiwa ameichezea klabu hiyo tangu akiwa na umri wa miaka 14 amekuwa akisomea ukocha kwa muda mrefu ambapo tayari amepata shahada mbalimbali za UEFA huku akiwa anamalizia shahada yake ya mwisho ambayo ni UEFA Pro License .
Giggs akiwa na umri wa miaka 40 ni mchezaji mwenye umri mkubwa kuliko wote ndani ya United na ana rekodi ya kuwa mchezaji pekee aliyefunga mabao kwenye kila msimu wa Ligi kuu ya England tangu ilipoanzishwa mwaka 92 na uteuzi wake unamaanisha kuwa atakuwa akifanya kazi yake kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo huku akibakia kuwa mhezaji baada ya kusaini nyongeza ya mkataba wa mwaka mmoja mwezi wa nne mwaka huu.
Akiwa amecheza zaidi ya 1000 za United kwenye kiwango cha juu uzoefu wa Giggs utakuwa silaha muhimu kwa kocha mpya David Moyes ambaye ndio kwanza ameanza kazi ya kuifundisha United Jumatatu ya wiki hii akiwa ameteuliwa kuchukua nafasi ya Sir Alex Fergusson aliyestaafu baada ya msimu uliopita akiwa amekaa kwenye benchi la United kwa miaka 26 .
Uteuzi huu unaweza kuwa mwanzo wa maisha mapya ya Giggs kwenye tasnia ya ukocha  pale atakapoamua kustaafu kucheza soka kwani amekuwa akisomea ukocha kwa muda mrefu na tayari ana vyeti vya kutosha na nafasi hii mpya itamuongezea uzoefu ambao utamfanya kuwa moja ya mahaguo ya kwanza kurithi nafasi ya David Moyes pale atakapofikia mwisho wake kama kocha .
Zaidi ya Giggs mchezaji wa zamani wa United ambaye alikuwa nahodha wa Everton wakati David  Moyes akiwa kocha mkuu Phil Neville anatarajiwa kujiunga na benchi la ufundi la United baada ya kutangaza kustaafu kucheza soka msimu uliopita.
Neville naye ana uzoefu wa ukocha akiwa amewahi kufanya kazi kama mmoja wa makocha wasaidizi wa timu ya taifa ya England kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 21 na kama Giggs amekuwa akisomea kozi kadhaa za ukocha ambazo amefuzu akiwa anashikilia shahada za UEFA B na UEFA A  . Neville mwenye umri wa miaka 36  aliichezea United kwa muda wa miaka 10 tangu mwaka 1995 mpaka 2005 ambapo alicheza mechi 263 kabla ya kuhamia Everton alikocheza kwa miaka 10 alipocheza mechi 242 kabla ya kustaafu mwishoni mwa msimu uliopita .

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...