facebook likes

Thursday, July 4, 2013

Ebwana Brazil wamepanda kwenye viwango vya soka Duniani, Tanzania je?



.
.
Ushindi ilioupata timu ya taifa ya Brazil kwenye michuano ya kombe la mabara mwishoni mwa wiki iliyopita umeisaidia timu hiyo kupanda zaidi ya nafasi kumi kwenye viwango vya ubora vya soka vya FIFA.
Brazil ilianza michuano hiyo ikiwa inashika nafasi ya 22 ambayo ni nafasi ya chini kuwahi kushikiliwa na timu hiyo lakini ushindi kwenye michezo yake mitano kuanzia hatua ya makundi, nusu fainali na fainali umeipandisha Brazil hadi kufikia nafasi ya tisa .
Bado Hispania wameendelea kushika nafasi ya kwanza wakifuatiwa na Ujerumani huku Colombia,Argentina na Uholanzi zikikamilisha orodha ya timu tano bora za dunia.
Italia ambao walifika hatua ya nusu fainali kwenye kombe la Mabara wanashika nafasi ya sita mbele ya Ureno walio kwenye nafasi ya saba huku Croatia , Brazil na Ubelgiji wakishika nafasi za nane, tisa na kumi .
.
.
Timu ya taifa ya Ivory Coast ambayo mchezo wake wa mwisho wa kimataifa ulikuwa dhidi ya Taifa Stars ya Tanzania ambapo Tembo hao walishinda kwa 4-2 wanabakia kuwa timu inayoshika nafasi ya kwanza kwa Afrika wakiwa wameshika nafasi ya 13 kwenye viwango vya dunia wakifuatiwa na Ghana walioko kwenye nafasi ya 24.
Mali ndio timu ya tatu kwa ubora Afrika wakiwa  wanawafuatia na Ghana  kwenye nafasi ya 28 huku tano Bora ikikamilishwa na Algeria na Nigeria wanaoshika nafasi za 4 na 5 wakiwa wameshika nafasi za 34 na 35 kimpangilio kwenye viwango hivyo.
Kwenye ukanda wa CECAFA ambako Tanzania iko ,Uganda wako kwenye nafasi ya juu wakiwa wanashikilia namba 19 kwa Afrika na 80 kidunia wakifatiwa na Ethiopia walio nafasi ya 25 kwa Bara la Afrika na nafasi ya 90 Duniani.
Tanzania inashika nafasi ya 35 kwenye orodha ya nchi 54 za Afrika huku ikiwa kwenye nafasi ya 121 Duniani.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...