facebook likes

Saturday, October 12, 2013

ACTRESS HIDAYA NJAIDI AOMBA MSAADA WA KUTIBIWA MKONO WAKE NJE YA NCHI.


  Hidaya Njaidi
Muigizaji wa filamu Swahiliwood anayeuvaa uhusika wa mama katika filamu nyingi, Hidaya Njaidi aliyepata ajali mwanzoni mwa mwaka huu na kuumia vibaya mkono anaomba msaada wa matibabu kwani mkono wake umesagika kwa ndani na anahitaji kupatiwa matibabu zaidi nje ya nchi.
SOMA ZAIDI..........
Akizungumza na Globalpublishers hivi karibuni, Hidaya alisema kuwa kwa sasa mkono wake unamuuma sana na anachosubiri ni kujua kiasi cha pesa anachotakiwa kutoa na hospitali atakayokwenda kutibiwa kati ya India au Afrika Kusini.
“Wiki ijayo ndiyo nitajua baada ya kurudi Muhimbili lakini ukweli ni kwamba mkono unanisumbua. Hata hivyo, sina pesa za kutosha hivyo naomba watu wanisaidie,” alisema Hidaya ambaye ameng'ara sana na filamu nyingi.
Get well soon Hidaya......    

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...