facebook likes

Thursday, July 11, 2013

suala la ubakaji watoto zanzibar bado halijachukuliwa hatua za kutosha-Baraza la wawakilishi zanzibar.

Imeelezwa kuwa Jeshi la Polisi na Mahakama bado hawajalichukulia hatua za makusudi suala la ubakaji watoto ambalo linaonekana likiendelea kuengezeka siku hadi siku.  
Kutolichukulia hatua  huko ni pamoja na adhabu ndogo wanazo pewa wahalifu  na kutoridhishwa na ushahidi wa kuona unao tolewa na watu mbali mbali mahakamani.
 Hayo yamesemwa leo huko katika ukumbi wa  Baraza la wawakilishi  chukwani   wakati walipokuwa wakichangia bajeti ya Wizara ya Ustawi wa Jamii ,Vijana Maendeleo ya Wanawake na Watoto juu  ya suala zima la udhalilishaji na ubakaji  wa watoto  ulivyokithiri hapa nchini.
Wamesema hali hiyo mbaya  inatokana na jeshi   hilo na Mahakama kutochukua  hatua za makusudi za kisheria kwa watuhumiwa ambao wanahusika na kesi za uzalilishaji watoto na  na kuwachilia kuwapa adhabu ndogo au kuto kamilika ushahidi wakuona.
 “Polisi wanataka ushahidi  wa aina gani ? kila siku suala la ubakaji linaongezeka hivi karibuni mtu kafungwa miezi sita kwa kosa la ubakaji hio ni adhabu ndogo  kulingano na kosa lenyewe, alisema mmoja wawalikilishi hao.
Aidha walisema kuwa masuala ya udhalilishaji yanafanywa na watu wazima wenye akili zao timamu jambo ambalo linawasababisha   watoto hao kuona aibu  na kuweza kuathirika kisaikolojia .

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...