facebook likes

Thursday, July 11, 2013

POLISI YAWAZUIA CHADEMA KUANZISHA KAMBI YA KIJESHI KWA AJILI YA KUWAANDAA VIJANA WAKE



Mnamo tarehe 09/07/2013, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe, Freeman Mbowe alitoa kauli kwamba wanaunda kikundi chao cha kuwalinda ambacho watakipatia mafunzo ya ukakamavu.



Kitendo cha chama chochote cha siasa ikiwemo CHADEMA kuanzisha kikundi cha kujihami ni kinyume cha sheria za nchi na endapo watafanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.



Kufuatia kauli hiyo, Jeshi la Polisi nchini limeanza uchunguzi na litachukua hatua kulingana na ushahidi utakaopatikana. Aidha, Jeshi la Polisi litamshughulikia mtu yeyote atakayekwenda kinyume cha sheria bila kujali wadhifa wake.

Imetolewa na:-

Advera Senso-SSP

Msemaji wa Jeshi la Polisi.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...