DAR ES SALAAM.  
MAKACHERO wa Marekani 
wameendelea na matayarisho ya mwisho ya ziara ya Rais Barack Obama, 
ambapo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere walikuwa na
 kazi ya kuunganisha helikopta za doria.
Makachero hao walikuwa wakiunganisha helikopta 
sita zilizosafirishwa vipande vipande kutoka Marekani, ambapo meli mbili
 za kivita na ndege moja pia zimewasili.
Rais Obama tayari yuko katika ardhi ya Afrika, 
ambapo leo anatarajiwa kwenda Afrika Kusini baada ya kumaliza ziara yake
 ya kwanza Senegal na anatar
ajiwa kuwasili nchini Jumatatu.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa jana na 
Mwananchi unaonyesha Marekani imeleta helikopta hizo kwa ajili ya ulinzi
 wa Rais Obama, zikiwemo meli zilizobeba helikopta nyingine mbili na 
ndege.
Habari zilizopatikana kutoka kwa wafanyakazi wa 
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,zinasema kuwa helikopta 
sita zinaunganishwa katika sehemu ya karakana ya Kikosi cha Anga cha 
Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Mpashaji mmoja aliliambia gazeti hili kuwa 
helikopta hizo zililetwa kama vipande vipande vilivyosafirishwa kama 
mzigo kwenye meli za kivita zilizotia nanga jijini Dar es Salaam.
“Nilikaribia kwenye eneo la karakana na 
nikashangaa kuona jinsi jamaa walivyokuwa ‘bize’ wakiunganisha vyuma 
mbalimbali na kutengeneza helikopta hizo,” aliongeza mpashaji wetu, 
ambaye alibahatika kusogelea eneo hilo licha ya kuwepo kwa ulinzi mkali.
Inaaminika kuwa helikopta hizo zitakuwa zinasaidia
 kusafirisha watu na mizigo kutoka kwenye meli za kivita ambazo 
zimeegeshwa kwenye Kikosi cha Maji cha JWTZ.
Pia helikopta mbili zinaaminika ziko katika meli ambazo zimeegeshwa huko Kigamboni.
Meli za kivita na ndege ya kijeshi
Katika hatua nyingine, meli mbili za kivita ambazo zimetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu zimeegeshwa Kigamboni.
“Jamaa wana meli kali kwa kweli, mimi nimekuwa 
askari wa Kikosi cha Maji kwa muda mrefu na kufanya mazoezi na mataifa 
kadhaa, lakini sijaona meli kama zile.
CHANZO MWANANCHI. 

No comments:
Post a Comment