facebook likes

Friday, February 15, 2013

TAARIFA KUHUSU MWANARIADHA ALIEMUUA MPENZI WAKE SIKU YA VALENTINE


.
Polisi wa Afrika Kusini wamethibitisha kwamba mwanariadha raia wa nchi hiyo Oscar Pistorius (26) atafikishwa Mahakamani february 15 2013 baada ya mpenzi wake kupatikana nyumbani kwake akiwa amefariki kwa kupigwa risasi feb 14 2013.

Wengi wamemfahamu kupitia michuano ya Olympic 2012 ambayo aliiwakilisha nchi yake na kushinda medali ya dhahabu.


Oscar akiwa chini ya ulinzi wa polisi.
Polisi wanasema inaaminika mpenzi wake Oscar aitwae Reeva Steenkamp (30) ambae ni model alipigwa risasi mara nne katika sehemu mbalimbali za mwili wake nyumbani kwa Oscar.
Pia wamesema kuna taarifa za kifo hicho kusababishwa na suprise aliyoifanya Reeva katika siku hiyo ya wapendanao, inadaiwa alikwenda nyumbani kwa Oscar kwa kushtukiza hivyo Oscar bila kupata uhakika alianza kufyatua risasi akidhani kavamiwa na majambazi.
Mapenzi ya Oscar na Reeva yalianza November 2012 ambapo hata Reeva mwenyewe hakuficha upendo wake mkubwa alionao kwa Oscar alipohojiwa na Sunday Times wiki iliyopita, na  katika tweets zake za mwisho Reeva alionekana kuwa ameipania siku ya wapendanao huku akisisitiza kwamba ni siku ya upendo kwa kila mmoja.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...