facebook likes

Friday, September 27, 2013

Kuhusu maziko ya Wanajeshi na huyu Mtangazaji waliouwawa kwenye shambulio la Westgate Kenya

36
SOMA ZAIDI.......
Mwanajeshi wa kwanza alieuwawa
1. Isaya Kibet Terer ni mmoja wa Wanajeshi waliopoteza maisha kwenye harakati za kuokoa watu waliokua wametekwa kwenye jumba la kibiashara la Westgate Nairobi Kenya.
2. Ni Mwanajeshi aliekua na miaka miwili tu toka aingie jeshini, alikua anafanya biashara pia ambapo alikua na daraja la Uluteni jeshini na umri wake ulikua miaka 23 tu lakini pia alikua anategemewa kuisaidia familia yake.
3. Kingine kumuhusu Mwanajeshi huu ambae alikua miongoni mwa Wanajeshi 11 waliojeruhiwa kwenye harakati za uokoaji ni kwamba alikua afunge ndoa mwezi December mwaka huu.
Mwanajeshi wa pili aliyeuwawa:
Onyango Opodi ambae alikua Luteni ni miongoni mwa Wanajeshi waliouwawa kwenye uokoaji kwenye jumba la Westgate ambapo kifo chake kimetokea siku tatu tu baada ya Mwanajeshi huyu kurudi Kenya akitokea Somalia alikokua amejiunga na jeshi la Kenya kwenye Opareshen.
Ruhila 1Mtangazaji Ruhila Adatya:
Ni miongoni mwa waliofariki kwenye shambulio la Westgate ambapo alifariki dunia akiwa na ujauzito njiani akikimbizwa hospitali baada ya kupata majeraha yaliyotokana na shambulio la magaidi Westgate.
Adatya alikua akiandaa kipindi cha mapishi cha TV kilichokua kinafanyika kwenye jumba hilo la Westgate ambapo kilikua ni shindano la Watoto kushindana kupika.
Mmoja wa mashuhuda amesema mtangazaji huyu wa East FM, Kiss TV, X Fm, Kiss 100 na E News.
Ruhila Adatya

source:millardayo.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...