facebook likes

Saturday, February 23, 2013

HUYU NDIO MDOGO WAKE BEYONCE WA NJE YA NDOA AMBAE BEYONCE AMEGOMA KUMUONA.


.
Unaambiwa stori za kuaminika zinatiririsha kwamba mwimbaji star wa dunia Beyonce amekataa kabisa kuonana na mdogo wake wa kiume aitwae Nixon (3) ambae baba mzazi wa Beyonce amempata na mwanamke mwingine wa nje ya ndoa aitwae Alexandra Wright.
Hiyo ni moja ya sababu kuu ambazo inadaiwa ndio zilivunja uhusiano kati ya mzee Knowles na mama Knowles pamoja na kina Beyonce huku za kuaminika zikipasha zaidi kwamba ndio kilikua chanzo cha Beyonce pia kujiondoa kuwa chini ya baba yake kikazi manake mwanzoni Knowles ndio alikua meneja wa Beyonce.

Nixon na baba yake mzazi mzee Knowles mwenyewe.

The Box wameripoti pia kwamba uhusiano wa mzee Knowles na Alexandra ndio uliivunja ndoa yake na Tina ambae ndio mama mzazi wa Beyonce ambapo star Magazine wameripoti tena kwamba Beyonce hana furaha na baba yake sasa hivi kwa hiyo dhambi aliyofanya baada ya ndoa yake kudumu kwa miaka 31.
Pamoja na kwamba mzee Knowles aliamua kuhamia kwa nyumba ndogo na kuamua kuzaa mtoto mmoja, mke wa nyumba ndogo ambae ni Alexandra amesema uhusiano wake na Knowles ulikua wa miezi 18 tu ambayo waliishi pamoja ila baada ya hapo mzee akaanza kuzingua wakati Alexandra akiwa mjamzito na hata alipojifungua mzee akamtelekeza.

Beyonce na mama mzazi.

Pamoja na kwamba mzee huyu alimkataa huyu mtoto wa nje, vipimo vilionyesha kwamba mtoto ni wake kabisa ambapo Mahakama moja Los Angeles Marekani ilimuamuru atoe dola elfu 8,200 kama matunzo ya mtoto.
Mzee Knowles ni mmoja kati ya wenye heshima kwenye muziki, ndio mtu aliyegundua kipaji cha Beyonce na hata kuunda kundi la Destiny’s Child, one of the biggest girl groups of all time.
Beyonce sio staa wa kwanza kusikia kwamba hapatani au haongei na baba yake, imeshatokea kwa Kelly Rowland pia na hata movie star ambae amewahi kuja Tanzania kwenye mbuga za wanyama na kulala kwenye hoteli namba moja duniani Angelina Jolie.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...