facebook likes

Wednesday, September 18, 2013

Uganda Kuwaadhibu Wanajeshi Wake

Siku ya Jumatatu serikali ya Uganda iliwasimamisha wanajeshi 24 wanaohudumu kwenye Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) kwa tuhuma za kuuza chakula na mafuta kilichokusudiwa wanajeshi wa Uganda kwa njia ya magendo.
SOMA ZAIDI....
Kamanda wa kikosi cha Uganda, Brigedia Michael Ondoga, alikuwa miongoni mwa walioitwa nyumbani na Rais Yoweri Museveni, ambaye pia alifuta uteuzi mpya wa Ondoga kama mwambata wa kijeshi katika balozi jijini Nairobi, liliripoti gazeti la Daily Monitor la Uganda.
Wanajeshi wa Uganda waliopelekwa kama walinda amani nchini Somalia walikuwa kila mara wakila mlo mmoja tu kwa siku kwa sababu ya kashfa hiyo, uchunguzi wa gazeti hilo ulibainisha mwezi Juni.
Wanajeshi waliosimamishwa kazi walitarajiwa kurudi Uganda siku ya jana kukabiliana na kesi kwenye mahakama ya kijeshi.
"Hatima yao ilitokana na uchunguzi," msemaji wa wizara ya ulinzi ya Uganda, Paddy Nkunda, aliliambia shirika la habari la AFP. "Ikiwa ushahidi wa kutosha utakusanywa, basi maafisa hao watapelekwa mahakamani."




source:djsek

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...