facebook likes

Sunday, July 28, 2013

ANCELOTTI AMPAMBA RONALDO.


MENEJA mpya wa klabu ya Real Madrid Carlo Ancelotti amemuelezea Cristiano Ronaldo kama mchezaji wa kipekee kuliko wote ambao amewahi kuwafundisha. Ancelotti amesema amefundisha wachezaji wengi wenye vipaji lakini Ronaldo ni tofauti kwasababu ana kipaji cha kipekee na nguvu, kila kocha lazima afurahie kumfundisha mchezaji huyo. Kocha aliendelea kudai kuwa Ronaldo ni mchezaji mwenye weledi na ana uhakika atakuwa na msimu wenye mafanikio katika kipindi cha 2013-2014. Ronaldo alimaliza katika nafasi ya pili katika orodha ya wafungaji kwenye La Liga msimu uliopita akiwa amefunga mabao 34 katika mechi 34 alizocheza akiwa amepitwa na mshindi wa tuzo ya Ballon r’Or Lionel Messi ambaye alifunga mabao 46.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...