facebook likes

Thursday, February 21, 2013

BARABARA YA OLD BAGAMOYO SASA KUITWA MWAI KIBAKI


Barabara iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Old Bagamoyo kuanzia leo itaanza kuitwa jina la 'Mwai Kibaki road' ikiwa ni heshima kwa aliyotunukiwa rais huyo wa Kenya kwa ziara yake ya siku mbili nchini hapa.

Mkuu mkoa wa Dar es salaam Meck Sadik amesema barabara hiyo yenye urefu wa Km 10.1 ni kuanzia kwenye mataa ya Morocco hadi mzunguko wa kuelekea Africa Mbezi beach mkabala na uwanja wa JWTZ.

Pia Rais Mwai Kibaki atatumia fursa hiyo kuwaaga na kuwashukuru watanzania kwa ushirikiano wao kipindi cha uongozi wake maana muhula wa uongozi wake unaelekea kikomo hapo baadaye mwaka huu.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...