facebook likes

Thursday, August 22, 2013

FURSA NDANI YA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA MAPEMA LEO MKOANI TABORA.

 Msanii wa Muziki wa kughani Mashairi, Mrisho Mpoto,akibadilishana mawazo na baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Media Group muda mfupi baada ya kumaliza kutoa soma la Kamata Fursa Twenzetu ndani ya ukumbi wa Chuo cha fursa ya chuo cha utumishi wa umma mkoani Tabora mapema leo.
SOMA NA ANGALIA PICHA ZAIDI........
 "Mnanionaaaa.."! Mpoto akiwa amembeba mmoja wa wanafunzi wa Chuo hicho mara baada ya kumuomba apige naye picha ya kumbukumbu.
 Baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho wakiwa wamejitokeza kwa wingi wakitaka kupiga picha na Mrisho Mpoto mapema leo.
 Wanafunzi hao pia walipata fursa ya kupiga picha na Mpoto.
 Baadhi ya wanafunzi wakisikiliza mafunzo ya Kamata Fursa Twenzetu katika chuo hicho.
 Mpoto akitoa somo kwa wanafunzi hao mapema leo katika ukumbi wa Chuo hicho.
  Somo la Mpoto liliambatana na mifano hai ambayo ilikuwa ikiwasisimua vilivyo Wanafunzi hao.
Mtangazaji wa Clouds FM kupitia kipindi cha Power Break fast Gerald Hando naye alipata wasaa wa kuzungumza na wanafunzi hao kuhusiana na mpango mzima wa tamasha la Serengeti Fiesta 2013 linalotarajiwa kufanyika kesho jioni kwenye uwanja wa Al-Hassan Mwinyi,aidha pia alibadilishana nao mawazo na  namna ya kutumia fursa mbalimbali wazipatazo katika masoma yao.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...