facebook likes

Tuesday, February 19, 2013

MATOKEO FORM IV: IDADI YA WALIOFAULU NA WALIOFELI IKO HAPA.



Hii picha ilipigwa Meru Arusha january 2013.
Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi february 18 2013 imetangaza matokeo ya kidato cha nne 2012 ambapo yameonyesha kiwango cha kufaulu kimeshuka kwa asilimia kubwa ikilinganishwa na miaka iliyopita.
Waziri wa wizara hiyo Dr. Shukuru Kawambwa amesema kati ya wanafunzi laki nne na elfu 56 waliofanya mtihani, wanafunzi laki mbili na elfu 40 sawa na nusu ya wote waliofanya mtihani, wamefeli kwa kupata sifuri ambapo pia matokeo yameonyesha shule binafsi zimeendelea kufanya vizuri ikilinganishwa na shule za serikali huku idadi ya kufaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu nayo ikishuka kwa zaidi ya asilimi 50.
Namkariri Dr Kawambwa akisema “Tathmini ya awali iliyofanywa kuhusu ufaulu wa Watahiniwa katika shule mbalimbali inaonyesha kuwa shule zilizofanya vizuri zaidi ni zile ambazo zina mahitaji yote ya msingi ikiwemo walimu wa kutosha, miundombinu iliyokamilika, vifaa vya kufundishia na kujifunzia vya kutosha, shule zenye ufaulu wa chini ni zile ambazo zina changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukosa walimu wa sayansi na hisabati kwa shule za vijijini, kutokuwepo kwa maabara kwa shule zenye mkondo wa sayansi na kutokuwepo kwa maabara kwa ajili ya kujisomea”
Waliopata division 1 ni wavulana elfu moja na sabini na tatu, wasichana ni mia tano 68 ambapo jumla yao ni 1641, division two wavulana ni elfu 4 mia 4 na 56 na wasichana ni elfu 1 mia 9 na 97 jumla yao ni elfu 6453, division three wavulana na elfu 10 mia 8 na 13 na wasichana ni elfu 4 mia 6 na 13 jumla yao ni elfu 15 mia 4 na 26, ukijumlisha divisio one mpaka three wavulana ni 16342 na wasichana 7178.
Katika mtihani huo jumla ya wanafunzi 728 wamefutiwa majibu ya mtihani wao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya udanganyifu pamoja na kutoa lugha chafu.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...